Saturday, July 11, 2015

NAPEATHIBITISHA 5 BORA CCM NI MEMBE, MAGUFULI, MIGIRO, MAKAMBA, NA AMINA SALUM ALI

Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nd. Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa White House, Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi mjini Dodoma. Katika taarifa yake amethibitisha taarifa zilizotawala vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuhusiana na mijina matano yaliyoteuliwa na kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika mchakato wa kumpata mgombea urais katika uchaguzi mkuu kwa tiketi ya chama hicho chenye nguvu katika siasa za Tanzania. Kwa mujibu wa Bw. Nape Nnauye, waliofuzu kuingia hatua ya tano bora ni 1). Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe; 2) Waziri wa Ujenzi, Mh. John Mgufuli; 3) Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Asha-Rose Migiro, 4) Naibu Waziri wa Mawasiliano, Mh. Januari Makamba, na 5). Balozi wa Kudumu wa Africa nchini Marekani, Mh. Amina Salum Ali

Majina hayo ndio yamekua agenda kuu kujadiliwa katika kikao cha Halmashauri kuu ya CCM ambapo maamuzi yataweka muafaka na kuwachuja kupata tatu bora ambayo itawasilishwa katika kikao cha Mkutano Mkuu takaofanyika katika ukumbi mya wa CCM mjini Dodoma na hatimaye kupatikana jina mija la ambaye atakuwa mgombea Urais katika uchaguzi mkuu wa  mwezi October mwaka huu.

No comments:

Post a Comment