Tuesday, September 29, 2015

CHADEMA WAENDELEA KUDHALILIKA KUTOKANA NA SABABU ZA KUHAIRISHA MIKUTANO YAO YA KAMPENI

CHADEMA WAENDELEA KUDHALILIKA KUTOKANA NA SABABU ZA KUHAIRISHA MIKUTANO YAO YA KAMPENI

Taarifa ya wazi kwa umma kufuatia taarifa ya CHADEMA kuhairisha mkutano


Hii ni baada ya kuhairishwa mkutano wa kampeni za CHADEMA/ UKAWA mjini Tanga ambapo taarifa za ndani za chama hicho zilisema kuwa mkutano huo ulihairishwa kutokana na wimbi kubwa la wanachama waliojitokeza katika viwqnja vya Tangamano jambo lililosababisha kushindwa kutua kwa Helkopta ya mgombea Urais wa chama hicho Edward N. Lowassa, ambapo ililazimika kwenda kutua uwanja wa ndege na ndipo mgombea huyo na msafara wake walifika viwanjani hapo kwa kutumia gari ziizoandaliwa kwa ajili yao. Taarifa hiyo ilieleza kwamba katika mkutano huo mkubwa sana kulikua na msongamano mkubwa uliosababisha wanachama wengi kuanguka na kupoteza fahamu (kuzimia) ambapo kitengo cha huduma ya kwanza kushindwa kumudu hali hiyo licha ya wagonjwa wengi kufikishwa hospitali mbalimbali. Hata hivyo katika mkutano huo mgombea huo wa Urais alihutubia umma huo kwa tariba dakika tatu tu kabla ya kuhairishwa na mgombea huyo kuwahishwa haraka katika dharura iliyomlazimu kuondoka uwanjani hapo. 



No comments:

Post a Comment