Wednesday, August 26, 2015

MJUE MGOMBEA UTAKAYEMPIGIA KURA october 25.


Kumekua na utamaduni ulijenga imani kwa jamii kuamini kwamba kura ni siri kwa mpigaji tu wa kura hizo. Lakini hali imekua tofauti kwa makada na hata mashabiki na wafuasi wa vyama mbali mbali hapa nchini.
Hili limedhihirika hasa pale makada na mashabiki vyama fulani vya siasa kuonesha misimamo yao waziwazi juu ya kuunga mkono chama ama mgombea wa chama fulani na kujivunia kua ushindi wa chama chake utasababiswa na yeye kuelekeza kura yake kwa chama hicho.
Kumekua na mijadala ya wazi tena wakati mwingine kwa mabishano, wakitaniana kuwa "mwaka huu nyie lazima muwanguke", ama "nyie mtaisoma namba" lakini pia kumekua na kujiamini na hata kutambiana kwamba "mgombea wetu jembe" ilimuradi tu kila mwanachama kudhihirisha kuwa kurake isiwe siri na ijulikane mapema misimamo ya yao ni kwa mgombea/ chama fulani.
Baadhi wa watumiaji wa mitandao ya kijamii wamefikia hata kuwafuta urafiki marafiki zao wa muda mrefu mitandaoni, kwa sababu tu ya kukithiri kuweka post/mada ama picha za kudhihirisha msimamo wao kisiasa.
Lakini kwa upande mwingine, kughihirisha kuunga mkono chama/mgombea fulani kumeonekana kuongeza uwazi katika nyanja hii ya siasa kwani hata wahombea ama chama huongeza nguvu kwa wanachama wake tu kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi, kuanzia kujiandikisha, kushiriki kwenye mikutano ya chama na kampeni na hata kuomba ridhaa ya uongozi.
Kuoelekea uchaguzi mkuu October 25 mwaka huu, mchuano mkali umejitokeza hasa kwa wagombea kiti cha Rais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM dhidi ya mpinzani wake wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.
Uchaguzi mkuu Tanzania hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo viongozi katika nafasi za Urais, Ubunge, Uwakilishi (Zanzibar) na Udiwani huchaguliwa kwa kuzingatia mfumo wa kidemokrasia za vyamba vingi.







No comments:

Post a Comment